Angalizo: Wiki mbili baada ya kutoa mimba, vipimo vitaendelea kuonyesha kua bado una ujauzito hii inatokana na homoni zilizoko ndani ya mwili wako. Kama bado unahisi dalili za ujauzito (maumivu ya matiti, kichefuchefu, uchovu n.k) baada ya kutumia vidonge, muone daktari.
Wakati mimba inavyotoka, dalili hap juu ni kawaida. Kuwa makini. Chini ni baadhi ya ishara kwamba unaweza kuwa katika hatari ya kupata matatizo makumbwa.
Iwapo utajaza vitamba viwili vya hedhi kwa masaa mawili mfululizo baada ya kudhania kwamba ushaavya mimba, hii ni ishara ya kufuja damu kwa wingi.Unatakiwa kupata msaada wa kitabibu kama unatoka damu nyingi kiasi hiki. Kuloanisha pedi inamaanisha pedi kubwa yote imeloana damu mbele na nyuma, pembeni na pembeni na juu mpaka chini.
Maumivu Makali:Kama unapata maumivu makali sana ambayo hayapungui hata baada ya kunywa dawa ya Ibuprofen, pata msaada wa kitabibu. Maumivu makali sana huenda ikamaanisha umepata matatizo makubwa ya mimba. Maumivu yasiyopungua ambayo hayapungui hata baada ya kunywa dawa ya Ibuprofen inaweza kuwa dalili ya hatari. Tunashauri mwanamke yeyote mwenye mimba nayepata maumivu atafute msaada wa kitabibu.
Unajisikia kuumwa sana?: Unaweza kupata homa, kichefuchefu na kutapika siku ambayo umekunywa misoprostol ambayo ni kitu cha kawaida. Unatakiwa kujisikia nafuu zaidi kila siku baada ya kutumia vidonge vya kutoa mimba, na sio kuumwa. Kama utajisikia kuumwa Zaidi siku yoyote baada ya kumeza misoprostol unahitaji msaada wa kitabibu haraka.
References:
This website may require anonymous cookies and various third party services to function properly. You can read our Terms & Conditions and Privacy Policies. By continuing to use this site you are giving us your consent to do this.