Maswali kuhusu utoaji Mimba-Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Tembe za Kuavya Mimba

Nani Anaweza Kutumia Tembe za Kuavya Mimba?

    La, tumia idadi sawa ya tembe tunazopendekeza kwa kila mtu. Tafiti zinaonyesha kuwa ufanisi wa dawa haupungui kama una uzani zaidi . Hauhitaji kumeza kipimo tofauti au kumeza tembe Zaidi.

    Hauhitaji kubadili kipimo au idadi ya tembe ikiwa umegundua kuwa una mimba ya mapacha. Utaratibu unaofanana ndio hutumika kwa wanawake wenye mimba za mapacha.

    La, kila mimba ni tukio la kipekee. Ikiwa uliwahi kutumia tembe za kuavya mimba awali, hauhitaji kipimo zaidi ikiwa utaitumia tena kwa mimba tofauti isiyohitajika.

    Ikiwa una kidude cha kuzuia mimba katika tumbo la uzazi (kama vile koili au IUD ya progesterone ), ni lazima ukitoe kabla ya matibabu ya kuavya mimba

    Unaweza kunyonyesha kama kawaida wakati wa kutoa mimba kwa vidonge. Mifepristone na misoprostol zinaweza kuingia kwenye maziwa ya mama, lakini kiasi chake ni kidogo na haipaswi kusababisha madhara yoyote kwa mtoto. Ikiwa bado una hofu kuhusu hilo, unaweza kumnyonyesha mtoto, kutumia tembe za misoprostol, na kusubiri saa 4 kabla ya kunyonyesha tena. Ikiwa unahitaji kutumia vidonge vingine vya misoprostol, nyonyesha tena kabla ya kutumia vidonge. Walakini, hii ni chaguo lako kabisa na inategemea mapendeleo yako.

    Ikiwa unaishi na HIV, hakikisha kuwa uko hali dhabiti, unatumia dawa za kupunguza makali ya virusi, na kuwa afya yako ni nzuri.

    Kama una anemia (viwango vidogo vya madini ya chuma katika damu yako), tambua mhudumu wa afya asiye zaidi ya dakika 30 mbali nawe ambaye anaweza kukusaidia ukiitaji msaada. Ikiwa umezidiwa na anemia, tafuta ushauri wa daktari kabla ya kutumia tembe ya kuavya mimba.

    La, kutumia tembe za kuavya mimba mapema unapokuwa mja mzito ni salama hata kama ulijifungua kwa njia ya upasuaji.

    Hakuna uhusiano ambao umepatikana kati ya mifepristone na kasoro za kuzaliwa. Hata hivyo misoprostol huwa inasababisha kiwango kidogo cha ongezeko za kasoro za kuzaliwa. Kama utameza misoprostol na bado ungali mja mzito baada ya kumeza tembe, unaweza kupoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa hautapoteza mimba hiyo na uwe nayo hadi wakati utimie, hatari ya kasoro za kuzaliwa huongezeka kwa 1% (mtoto mmoja kwa kila 100).

    La, si salama kutumia tembe za kuavya mimba ikiwa unajua kuwa uko katika hatari ya kuwa na ujauzito usio katika tumbo la uzazi. Kwa sababu ulikatwa mirija ya uzazi, tunajua kuna kovu katika mrija (futuza). Hiyo ndio maana labda ujauzito wako wa mwisho ulitokea nje ya tumbo la uzazi. Futuza ndipo yai la mwanamke linarutubishwa na mbegu za kiume. Ujauzito unaanza kukua na husafiri katika mrija hadi tumbo la uzazi. Ikiwa mrija wako una kovu, ujauzito wa awali unaweza ukanaswa katika mrija. Ujauzito unapokua, unaweza kusababisha mrija kupasuka. Ikiwa mrija utapasuka, hii inaweza kusababisha umwagikaji wa damu ndani yako, na ni tishio kwa maisha yako. Uko katika hatari ya kupata ujauzito mwingine nje ya tumbo la uzazi. Haustahili kutumia tembe za kuavya mimba mwenyewe hadi ufanye kipimo cha ultrasound na kuhakikisha kuwa ujauzito uko katika tumbo la uzazi na si katika mirija yako.

    Kwanza, unastahili kujua kuwa hauwezi kujua uko katika hali hii hadi ufanyiwe kipimo cha ultrasound. Ujauzito nje ya tumbo la uzazi hauwezi kudumu hivyo hata katika nchi ambapo uaviaji mimba ni kinyume cha sheria unaweza kufanyiwa utaratibu wa kisheria kwa kutamatisha huu ujauzito.

    Kama mwanamume aliyebadili jinsia ama mtu asiyejitambulisha na jinsia yoyote, ni salama kutoa mimba kwa kutumia tembe. Kama unatumia homoni za kiume, misoprostol ama mifepristone haitaziharibu. Hizi tembe za utoaji mimba zinaweza kutumiwa salama kama unatumia homoni (GnRH) za kuwachilia testosterone (T) na/ama gonadotrophin. Hata hivyo, unaweza kukumbana na ugumu wa kupata utunzaji jumuishi wa utoaji mimba. Jifunze zaidi kuhusu utunzaji wa kutoa mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

Nani Anaweza Kutumia Tembe za Kuavya Mimba?

    La, tumia idadi sawa ya tembe tunazopendekeza kwa kila mtu. Tafiti zinaonyesha kuwa ufanisi wa dawa haupungui kama una uzani zaidi . Hauhitaji kumeza kipimo tofauti au kumeza tembe Zaidi.

    Hauhitaji kubadili kipimo au idadi ya tembe ikiwa umegundua kuwa una mimba ya mapacha. Utaratibu unaofanana ndio hutumika kwa wanawake wenye mimba za mapacha.

    La, kila mimba ni tukio la kipekee. Ikiwa uliwahi kutumia tembe za kuavya mimba awali, hauhitaji kipimo zaidi ikiwa utaitumia tena kwa mimba tofauti isiyohitajika.

    Ikiwa una kidude cha kuzuia mimba katika tumbo la uzazi (kama vile koili au IUD ya progesterone ), ni lazima ukitoe kabla ya matibabu ya kuavya mimba

    Unaweza kunyonyesha kama kawaida wakati wa kutoa mimba kwa vidonge. Mifepristone na misoprostol zinaweza kuingia kwenye maziwa ya mama, lakini kiasi chake ni kidogo na haipaswi kusababisha madhara yoyote kwa mtoto. Ikiwa bado una hofu kuhusu hilo, unaweza kumnyonyesha mtoto, kutumia tembe za misoprostol, na kusubiri saa 4 kabla ya kunyonyesha tena. Ikiwa unahitaji kutumia vidonge vingine vya misoprostol, nyonyesha tena kabla ya kutumia vidonge. Walakini, hii ni chaguo lako kabisa na inategemea mapendeleo yako.

    Ikiwa unaishi na HIV, hakikisha kuwa uko hali dhabiti, unatumia dawa za kupunguza makali ya virusi, na kuwa afya yako ni nzuri.

    Kama una anemia (viwango vidogo vya madini ya chuma katika damu yako), tambua mhudumu wa afya asiye zaidi ya dakika 30 mbali nawe ambaye anaweza kukusaidia ukiitaji msaada. Ikiwa umezidiwa na anemia, tafuta ushauri wa daktari kabla ya kutumia tembe ya kuavya mimba.

    La, kutumia tembe za kuavya mimba mapema unapokuwa mja mzito ni salama hata kama ulijifungua kwa njia ya upasuaji.

    Hakuna uhusiano ambao umepatikana kati ya mifepristone na kasoro za kuzaliwa. Hata hivyo misoprostol huwa inasababisha kiwango kidogo cha ongezeko za kasoro za kuzaliwa. Kama utameza misoprostol na bado ungali mja mzito baada ya kumeza tembe, unaweza kupoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa hautapoteza mimba hiyo na uwe nayo hadi wakati utimie, hatari ya kasoro za kuzaliwa huongezeka kwa 1% (mtoto mmoja kwa kila 100).

    La, si salama kutumia tembe za kuavya mimba ikiwa unajua kuwa uko katika hatari ya kuwa na ujauzito usio katika tumbo la uzazi. Kwa sababu ulikatwa mirija ya uzazi, tunajua kuna kovu katika mrija (futuza). Hiyo ndio maana labda ujauzito wako wa mwisho ulitokea nje ya tumbo la uzazi. Futuza ndipo yai la mwanamke linarutubishwa na mbegu za kiume. Ujauzito unaanza kukua na husafiri katika mrija hadi tumbo la uzazi. Ikiwa mrija wako una kovu, ujauzito wa awali unaweza ukanaswa katika mrija. Ujauzito unapokua, unaweza kusababisha mrija kupasuka. Ikiwa mrija utapasuka, hii inaweza kusababisha umwagikaji wa damu ndani yako, na ni tishio kwa maisha yako. Uko katika hatari ya kupata ujauzito mwingine nje ya tumbo la uzazi. Haustahili kutumia tembe za kuavya mimba mwenyewe hadi ufanye kipimo cha ultrasound na kuhakikisha kuwa ujauzito uko katika tumbo la uzazi na si katika mirija yako.

    Kwanza, unastahili kujua kuwa hauwezi kujua uko katika hali hii hadi ufanyiwe kipimo cha ultrasound. Ujauzito nje ya tumbo la uzazi hauwezi kudumu hivyo hata katika nchi ambapo uaviaji mimba ni kinyume cha sheria unaweza kufanyiwa utaratibu wa kisheria kwa kutamatisha huu ujauzito.

    Kama mwanamume aliyebadili jinsia ama mtu asiyejitambulisha na jinsia yoyote, ni salama kutoa mimba kwa kutumia tembe. Kama unatumia homoni za kiume, misoprostol ama mifepristone haitaziharibu. Hizi tembe za utoaji mimba zinaweza kutumiwa salama kama unatumia homoni (GnRH) za kuwachilia testosterone (T) na/ama gonadotrophin. Hata hivyo, unaweza kukumbana na ugumu wa kupata utunzaji jumuishi wa utoaji mimba. Jifunze zaidi kuhusu utunzaji wa kutoa mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

Aina za Tembe za Kuavya Mimba na Matumizi zao

    Utafiti unaonyesha kuwa utoaji mimba kwa matibabu inapendekezwa mara nyingo kwa mimba kabla ya wiki 13 tangu hedhi yako ya mwisho. Utaratibu wa HowToUseAbortionPill imetolewa kwa ajili ya mimba hadi wiki 13.Temeb za kutoa mimba zinaweza kutumika kwa mimba kubwa zaidi ya hio, lakini itahitaji taratibu na mazingatio tofauti kw usalama. Kwa taarifa zaidi, unaweza wasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi ili kujifunza zaidi kuhusu rasilimali za utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Utoaji mimba kwa tembe ni salama mno na una ufanisi sana ikitumiwa inavyofaa.Utoaji mimba kwa kutumia mifepristone na misoprostol hufaulu kwa zaidi ya asilimia 95, na uwezo wa matatizo kutokea huwa chini ya asilimia 1 kwa mimba ya hadi wiki 10 na asilimia 3 kwa mimba kati ya wiki 10 na 13.Ukitumia misoprostol pekee, utoaji mimba una kiwango cha kufaulu cha asilimia 80-85, na uwezo wa matatizo wa asilimia 1-4 kwa mimba ya hadi wiki 13. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, utoaji mimba kwa tembe unaweza kufanywa kwa usalama na ufanisi nyumbani, bora uwe na taarifa sahihi na unaweza kupata tembe zenye viwango bora.

    Marejeo:

    Kuna aina mbili ya tembe za kuavya mimba, na kila moja ina mbinu tofauti ya utenda kazi. Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa ujauzito, ilhali virutubishi vinavyotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa tumbo la uzazi (mwanya katika tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, na hivyo kusukuma ujauzito nje.

    Misoprostol husababisha tumbo la uzazi kujikaza na hivyo kutoa ujauzito.

    Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa mimba

    Ndio, unaweza kutumia misoprostol salama ukiwa nyumbani. Unapotumia tembe za misoprostol, jaribu kuhakikisha kuwa uko katika sehemu (kama kwako nyumbani) ambapo una ufaragha na unaweza kulala chini kwa saa chache baada ya kumeza tembe. Kuwa na mtu karibu nawe anayeweza kukuangalia na kukuletea chai moto au kitu cha kula inaweza kusaidia sana.

    Usinywe au kula kitu chochote kwa dakika 30 unaporuhusu misoprostol kuyeyuka. Baada ya dakika 30 kupita, unaweza kunywa maji ili kumeza mabaki ya tembe, na kwa jumla kiasi cha maji unachostahili ili kuhisi mwili una maji ya kutosha.

    Ndio, unaweza kunywa maji kukusaidia kumeza mifepristone.

    Kuna njia mbili za kutumia misoprostol: kuweka tembe katika uke wako au chini ya ulimi wako. HowToUseAbortionPill inapendekeza kuwa utumie tu misoprostol chini ya ulimi wako kwa sababu ni faragha zaidi (tembe huyeyuka haraka na haziachi mabaki yanayoonekana katika mwili wako) na huwa na hatari ndogo la ambukizo.

    Mchanganyiko wote wa jumla ya mifepristone na misoprostol na misoprostol pekee ndio tu chaguo yenye ufanisi. Hata hivyo, ikiwa inapatikana na unaweza kumudu gharama, mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol unastahili kuwa uamuzi wako unaopendelewa.

    Wanawake 98 kati ya 100 huwa na uaviaji mimba kamili ikiwa mifepristone na misoprostol zimetumika kwa pamoja. Takriban wanawake 95 kati ya 100 watakuwa na uaviaji mimba kamili ikiwa misoprostol pekee inatumika.

    Mifepristone na misoprostol hutumika pamoja kwa sababu tembe hizi hukamilishana. Mifepristone huzuia mimba kumea.Dawa inayotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa uzazi (kufungua tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, hivyo kusukuma nje ujauzito.

    Ikiwa utatumia tembe za misoprostol chini ya ulimi wako, hakuna mtu anaweza kujua kuwa ulitumia tembe za kuavya mimba kwa sababu utameza kila kitu baada ya dakika 30. Ikiwa mtu atauliza, unaweza kusema ulipoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa utatumia misoprostol kupitia uke, koti ya tembe huenda isiyeyuke kabisa kwa siku moja au mbili. Ikiwa unahitaji kutafuta usaidizi wa kiafya wa dharura kati ya saa 48 kwa sababu ulitumia misoprostol kupitia uke, mhudumu wa afya anaweza kuona koti nyeupe za tembe katika uke wako. Hii ndio maana HowToUseAbortionPill hupendekeza kutumia misoprostol chini ya ulimi wako na si ndani ya uke wako.

    Kama una mzio wa dawa za NSAID (ikiwemo ibuprofen), acetaminophen (Tylenol/Paracetamol) inapendekezwa kama dawa mbadala. Inapatikana katika duka za dawa katika nchi nyingi.Tumia tembe 2 (tembe za miligramu 325) kila saa 4-6 inavyohitajika kwa maumivu. Dozi ya juu sana katika saa 24 ni miligramu 400.

    Marejeo:

Aina za Tembe za Kuavya Mimba na Matumizi zao

    Utafiti unaonyesha kuwa utoaji mimba kwa matibabu inapendekezwa mara nyingo kwa mimba kabla ya wiki 13 tangu hedhi yako ya mwisho. Utaratibu wa HowToUseAbortionPill imetolewa kwa ajili ya mimba hadi wiki 13.Temeb za kutoa mimba zinaweza kutumika kwa mimba kubwa zaidi ya hio, lakini itahitaji taratibu na mazingatio tofauti kw usalama. Kwa taarifa zaidi, unaweza wasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi ili kujifunza zaidi kuhusu rasilimali za utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Utoaji mimba kwa tembe ni salama mno na una ufanisi sana ikitumiwa inavyofaa.Utoaji mimba kwa kutumia mifepristone na misoprostol hufaulu kwa zaidi ya asilimia 95, na uwezo wa matatizo kutokea huwa chini ya asilimia 1 kwa mimba ya hadi wiki 10 na asilimia 3 kwa mimba kati ya wiki 10 na 13.Ukitumia misoprostol pekee, utoaji mimba una kiwango cha kufaulu cha asilimia 80-85, na uwezo wa matatizo wa asilimia 1-4 kwa mimba ya hadi wiki 13. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, utoaji mimba kwa tembe unaweza kufanywa kwa usalama na ufanisi nyumbani, bora uwe na taarifa sahihi na unaweza kupata tembe zenye viwango bora.

    Marejeo:

    Kuna aina mbili ya tembe za kuavya mimba, na kila moja ina mbinu tofauti ya utenda kazi. Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa ujauzito, ilhali virutubishi vinavyotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa tumbo la uzazi (mwanya katika tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, na hivyo kusukuma ujauzito nje.

    Misoprostol husababisha tumbo la uzazi kujikaza na hivyo kutoa ujauzito.

    Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa mimba

    Ndio, unaweza kutumia misoprostol salama ukiwa nyumbani. Unapotumia tembe za misoprostol, jaribu kuhakikisha kuwa uko katika sehemu (kama kwako nyumbani) ambapo una ufaragha na unaweza kulala chini kwa saa chache baada ya kumeza tembe. Kuwa na mtu karibu nawe anayeweza kukuangalia na kukuletea chai moto au kitu cha kula inaweza kusaidia sana.

    Usinywe au kula kitu chochote kwa dakika 30 unaporuhusu misoprostol kuyeyuka. Baada ya dakika 30 kupita, unaweza kunywa maji ili kumeza mabaki ya tembe, na kwa jumla kiasi cha maji unachostahili ili kuhisi mwili una maji ya kutosha.

    Ndio, unaweza kunywa maji kukusaidia kumeza mifepristone.

    Kuna njia mbili za kutumia misoprostol: kuweka tembe katika uke wako au chini ya ulimi wako. HowToUseAbortionPill inapendekeza kuwa utumie tu misoprostol chini ya ulimi wako kwa sababu ni faragha zaidi (tembe huyeyuka haraka na haziachi mabaki yanayoonekana katika mwili wako) na huwa na hatari ndogo la ambukizo.

    Mchanganyiko wote wa jumla ya mifepristone na misoprostol na misoprostol pekee ndio tu chaguo yenye ufanisi. Hata hivyo, ikiwa inapatikana na unaweza kumudu gharama, mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol unastahili kuwa uamuzi wako unaopendelewa.

    Wanawake 98 kati ya 100 huwa na uaviaji mimba kamili ikiwa mifepristone na misoprostol zimetumika kwa pamoja. Takriban wanawake 95 kati ya 100 watakuwa na uaviaji mimba kamili ikiwa misoprostol pekee inatumika.

    Mifepristone na misoprostol hutumika pamoja kwa sababu tembe hizi hukamilishana. Mifepristone huzuia mimba kumea.Dawa inayotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa uzazi (kufungua tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, hivyo kusukuma nje ujauzito.

    Ikiwa utatumia tembe za misoprostol chini ya ulimi wako, hakuna mtu anaweza kujua kuwa ulitumia tembe za kuavya mimba kwa sababu utameza kila kitu baada ya dakika 30. Ikiwa mtu atauliza, unaweza kusema ulipoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa utatumia misoprostol kupitia uke, koti ya tembe huenda isiyeyuke kabisa kwa siku moja au mbili. Ikiwa unahitaji kutafuta usaidizi wa kiafya wa dharura kati ya saa 48 kwa sababu ulitumia misoprostol kupitia uke, mhudumu wa afya anaweza kuona koti nyeupe za tembe katika uke wako. Hii ndio maana HowToUseAbortionPill hupendekeza kutumia misoprostol chini ya ulimi wako na si ndani ya uke wako.

    Kama una mzio wa dawa za NSAID (ikiwemo ibuprofen), acetaminophen (Tylenol/Paracetamol) inapendekezwa kama dawa mbadala. Inapatikana katika duka za dawa katika nchi nyingi.Tumia tembe 2 (tembe za miligramu 325) kila saa 4-6 inavyohitajika kwa maumivu. Dozi ya juu sana katika saa 24 ni miligramu 400.

    Marejeo:

Hali ambayo tembe za kuavya mimba haizifai kutumiwa

    Unastahili kuepuka kutumia tembe za kuavya mimba nyumbani kwa kufuata utaratibu wa HowToUseAbortionPill ikiwa una ujauzito wa zaidi ya wiki 13; ikiwa unaathiriwa na mifepristone au misoprostol; una matatizo ya kina ya kiafya kama vile shida za kuganda kwa damu; au ikiwa unaamini au unajua kuwa ujauzito unakua nje ya tumbo la uzazi (ujauzito katika mrija wa uzazi)

Hali ambayo tembe za kuavya mimba haizifai kutumiwa

    Unastahili kuepuka kutumia tembe za kuavya mimba nyumbani kwa kufuata utaratibu wa HowToUseAbortionPill ikiwa una ujauzito wa zaidi ya wiki 13; ikiwa unaathiriwa na mifepristone au misoprostol; una matatizo ya kina ya kiafya kama vile shida za kuganda kwa damu; au ikiwa unaamini au unajua kuwa ujauzito unakua nje ya tumbo la uzazi (ujauzito katika mrija wa uzazi)

Madhara na Matatizo ya Tembe za Kuavya Mimba

    Kila utoaji mimba huwa tofauti. Unaweza kupata maumivi makali zaidi na kutokwa damu nyingi zaidi kushinda hedhi ya kawaida (ikiwa wewe huumwa wakati wa hedhi). Lakini pia ni kawaida kama utapata maumivu yasiyo makali na damu itoke tu kama vile hedhi ya kawaida. Madhara mengine ya kawaida ni kichefuchefu, kuhara,homa, na maumivu ya kichwa. Hata hivyo, unapaswa kuhisi nafuu chini ya saa 24. Ukianza kuhisi mgonjwa zaidi, basi tafuta msaada wa kimatabibu.

    Marejeo:

    Kwa baadhi ya watu, msokoto huwa mkali- zaidi ya msokoto wa hedhi (ikiwa una msokoto wa hedhi) na umwagikaji damu huwa zaidi ya ule wa hedhi. Unaweza kupitisha donge la damu hadi kiasi cha limau katika saa za kwanza baada ya kumeza misoprostol. Kwa wengine, msokoto huwa hafifu na umwagikaji wa damu huwa kawaida kama hedhi.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa hauna umwagikaji wa damu au una umwagikaji mdogo wa damu unaofuatwa na maumivu makali (hasa katika bega la kulia) ambayo hayapunguzwi na ibuprofen . Hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito ulio nje ya tumbo la uzazi. Ingawa ni nadra, inaweza kuwa tishio la maisha. Unaweza pia kuwafikia marafiki zetu katika www.safe2choose.org ili kuongea na mshauri wa uaviaji mimba aliye na mafunzo ikiwa unahisi kuwa uaviaji mimba haukufanikiwa.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa unalowesha visodo viwili vya hedhi kila saa kwa saa 2 mfululizo baada ya kufikiri ujauzito ushatoka. Kulowa kunamaanisha kuwa kisodo cha hedhi kimejaa damu mbele – hadi – nyuma, upande- hadi – upande na juu- hadi – chini.

    Meza tembe 3-4 (200 mg) za ibuprofen baada ya kila saa 6-8 ili kusaidia kuondoa maumivu yako. Kumbuka kuwa unaweza kumeza ibuprofen kabla ya kutumia misoprostol, pia

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kula unavyotaka. Vyakula vilivyokauka (kama vile vilivyookwa au kuchomwa) vinaweza kusaidia kichefuchefu, ilhali mboga, mayai na nyama nyekundu inaweza kurejesha madini yaliyopotea wakati wa kuavya mimba.

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kunywa kinywaji chochote unachokipenda (isipokuwa pombe).

    Pombe inastahili kuepukwa wakati wa mchakato wa utoaji mimba ili kuzuia kuathiri ufanisi wa dawa. Pombe inaweza kusababisha ongezeko la umwagikaji wa damu kutoka kwa tumbo la uzazi katika hali zingine na kupunguza ufanisi wa dawa zingine zinazomezwa kupunguza maumivu au ambukizo (ikiwa unakabiliana na matatizo). Kwa jumla, inapendekezwa kuepuka pombe hadi uthibitishe kuwa uaviaji mimba umekamilika na unahisi ukiwa na afya nzuri.

    Kwa wengi ujauzito utatoka baada ya saa 4-5 na kuhisi vyema chini ya saa 24. Ni kawaida kuendelea kuona umwagikaji mdogo wa damu na madoadoa hadi hedhi yako inayofuata takriban wiki 3-4.

    Ni kawaida kuhisi kuwa mgonjwa kwa tumbo lako, kuhara, kibaridi, au hata kuhisi una joto katika kipindi hiki. Wengi wanaripoti kuwa wanajua wakati mimba imetoka kwa sababu umwagikaji wa damu unapungua, na wanaanza kuhisi vyema zaidi.

    Matatizo katika utoaji mimba kwa matibabu ni nadra kabisa. Hata hivyo, ni muhimu uwe na uwezo wa kutambua dalili za matatizio. Kama utatokwa na damu nyingi (kulowesha taulo 2 za kawaida za hedhi kila saa moja kwa saa 2 mfululizo), una maumivu makali ambayo hayapungui baada ya kumeza ibuprofen au unaaza kujihisi mgonjwa siku yoyote baada ya kutumia misoprostol, unapaswa kutafuta ushauri wa kimatimabu.

    Je utoaji mimba kwa matibabu ama utoaji mimba nyumbani unakubaliwa na sheria katika nchi yako? Huenda utahitajika kuwa mwangalifu kuhusu kile utakachosema. Utoaji mimba kwa matibabu una dalilil sawa kama mimba kuharibika yenyewe ( pia inayojulikana kama mimba kutoka kwa hiari). Kwa hivyo, unaweza kusema vitu kama ‘natokwa damu,lakini sihisi kama ni hedhi yangu ya kawaida”

    Marejeo:

    Kuna njia tofauti za kujua kama utoaji mimba ulifaulu. Wakati wa utoaji mimba, unaweza kujua kama ulifikia vijinyama vya mimba ( vitafanana kama vile zabibu ndogo nyeusi kidogo na utando mwembamba au kifuko kidogo kilichozungukwa na utando mlaini mweupe) Hii ni ishara kuwa utoaji mimba ulifaulu. Hata hivyo, huenda haitakuwa rahisi kutambua vijinyama vya mimba. Ishara ingine ya utoaji mimba uliofaulu ni kupotea kwa dalili za mimba, kama vile ulaini wa matiti na kichefuchefu

    Kufanya kipimo cha mimba nyumbani pia ni njia ingine ya kuthibiti kufaulu kwa utoaji mimba. Hata hivyo, fahamu kwamba kipimo kinaweza kuonyesha mimba iko wiki 4 baada ya utoaji mimba, kwa sababu ya mabaki ya homoni mwilini mwako. Uchunguzi wa ultrasound utahitajika tu kama kuna mashaka ikiwa mimba ilifaulu kutoka ama kana kuna mashaka ya kuwepo kwa matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)

    Marejeo:

    Hauhitaji kufanya ultrasound baada ya kutoa mimba kutumia tembe. Ultrasound itahitajika tu ikiwa kuna mashaka ya matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)au ikiwa kuna mashaka kama mimba ilitoka. Kama utaendelea kuhisi dalili za mimba (ulaini wa matiti, kichefuchefu,uchovu n.k) baada ya kutumia tembe, utahitaji kushauriana na mhudumu wa afya kwa hatua za kufuata. Kuna uwezekano kuwa hatua inayofuata itakuwa uchunguzi wa ultrasound, kama itazingatiwa kufaa. Kwa taarifa zaidi, unaweza kuwasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi kujifunza zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Unaweza ukahitaji utaratibu wa upasuaji ikiwa bado una ujauzito baada ya kumeza tembe. Kumbuka! Matibabu ya uaviaji mimba usiyokamilika yanapatikana kwa urahisi popote duniani. Una haki kupata huduma hii, hata kama uaviaji mimba umebanwa kisheria katika nchi yako.

Madhara na Matatizo ya Tembe za Kuavya Mimba

    Kila utoaji mimba huwa tofauti. Unaweza kupata maumivi makali zaidi na kutokwa damu nyingi zaidi kushinda hedhi ya kawaida (ikiwa wewe huumwa wakati wa hedhi). Lakini pia ni kawaida kama utapata maumivu yasiyo makali na damu itoke tu kama vile hedhi ya kawaida. Madhara mengine ya kawaida ni kichefuchefu, kuhara,homa, na maumivu ya kichwa. Hata hivyo, unapaswa kuhisi nafuu chini ya saa 24. Ukianza kuhisi mgonjwa zaidi, basi tafuta msaada wa kimatabibu.

    Marejeo:

    Kwa baadhi ya watu, msokoto huwa mkali- zaidi ya msokoto wa hedhi (ikiwa una msokoto wa hedhi) na umwagikaji damu huwa zaidi ya ule wa hedhi. Unaweza kupitisha donge la damu hadi kiasi cha limau katika saa za kwanza baada ya kumeza misoprostol. Kwa wengine, msokoto huwa hafifu na umwagikaji wa damu huwa kawaida kama hedhi.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa hauna umwagikaji wa damu au una umwagikaji mdogo wa damu unaofuatwa na maumivu makali (hasa katika bega la kulia) ambayo hayapunguzwi na ibuprofen . Hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito ulio nje ya tumbo la uzazi. Ingawa ni nadra, inaweza kuwa tishio la maisha. Unaweza pia kuwafikia marafiki zetu katika www.safe2choose.org ili kuongea na mshauri wa uaviaji mimba aliye na mafunzo ikiwa unahisi kuwa uaviaji mimba haukufanikiwa.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa unalowesha visodo viwili vya hedhi kila saa kwa saa 2 mfululizo baada ya kufikiri ujauzito ushatoka. Kulowa kunamaanisha kuwa kisodo cha hedhi kimejaa damu mbele – hadi – nyuma, upande- hadi – upande na juu- hadi – chini.

    Meza tembe 3-4 (200 mg) za ibuprofen baada ya kila saa 6-8 ili kusaidia kuondoa maumivu yako. Kumbuka kuwa unaweza kumeza ibuprofen kabla ya kutumia misoprostol, pia

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kula unavyotaka. Vyakula vilivyokauka (kama vile vilivyookwa au kuchomwa) vinaweza kusaidia kichefuchefu, ilhali mboga, mayai na nyama nyekundu inaweza kurejesha madini yaliyopotea wakati wa kuavya mimba.

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kunywa kinywaji chochote unachokipenda (isipokuwa pombe).

    Pombe inastahili kuepukwa wakati wa mchakato wa utoaji mimba ili kuzuia kuathiri ufanisi wa dawa. Pombe inaweza kusababisha ongezeko la umwagikaji wa damu kutoka kwa tumbo la uzazi katika hali zingine na kupunguza ufanisi wa dawa zingine zinazomezwa kupunguza maumivu au ambukizo (ikiwa unakabiliana na matatizo). Kwa jumla, inapendekezwa kuepuka pombe hadi uthibitishe kuwa uaviaji mimba umekamilika na unahisi ukiwa na afya nzuri.

    Kwa wengi ujauzito utatoka baada ya saa 4-5 na kuhisi vyema chini ya saa 24. Ni kawaida kuendelea kuona umwagikaji mdogo wa damu na madoadoa hadi hedhi yako inayofuata takriban wiki 3-4.

    Ni kawaida kuhisi kuwa mgonjwa kwa tumbo lako, kuhara, kibaridi, au hata kuhisi una joto katika kipindi hiki. Wengi wanaripoti kuwa wanajua wakati mimba imetoka kwa sababu umwagikaji wa damu unapungua, na wanaanza kuhisi vyema zaidi.

    Matatizo katika utoaji mimba kwa matibabu ni nadra kabisa. Hata hivyo, ni muhimu uwe na uwezo wa kutambua dalili za matatizio. Kama utatokwa na damu nyingi (kulowesha taulo 2 za kawaida za hedhi kila saa moja kwa saa 2 mfululizo), una maumivu makali ambayo hayapungui baada ya kumeza ibuprofen au unaaza kujihisi mgonjwa siku yoyote baada ya kutumia misoprostol, unapaswa kutafuta ushauri wa kimatimabu.

    Je utoaji mimba kwa matibabu ama utoaji mimba nyumbani unakubaliwa na sheria katika nchi yako? Huenda utahitajika kuwa mwangalifu kuhusu kile utakachosema. Utoaji mimba kwa matibabu una dalilil sawa kama mimba kuharibika yenyewe ( pia inayojulikana kama mimba kutoka kwa hiari). Kwa hivyo, unaweza kusema vitu kama ‘natokwa damu,lakini sihisi kama ni hedhi yangu ya kawaida”

    Marejeo:

    Kuna njia tofauti za kujua kama utoaji mimba ulifaulu. Wakati wa utoaji mimba, unaweza kujua kama ulifikia vijinyama vya mimba ( vitafanana kama vile zabibu ndogo nyeusi kidogo na utando mwembamba au kifuko kidogo kilichozungukwa na utando mlaini mweupe) Hii ni ishara kuwa utoaji mimba ulifaulu. Hata hivyo, huenda haitakuwa rahisi kutambua vijinyama vya mimba. Ishara ingine ya utoaji mimba uliofaulu ni kupotea kwa dalili za mimba, kama vile ulaini wa matiti na kichefuchefu

    Kufanya kipimo cha mimba nyumbani pia ni njia ingine ya kuthibiti kufaulu kwa utoaji mimba. Hata hivyo, fahamu kwamba kipimo kinaweza kuonyesha mimba iko wiki 4 baada ya utoaji mimba, kwa sababu ya mabaki ya homoni mwilini mwako. Uchunguzi wa ultrasound utahitajika tu kama kuna mashaka ikiwa mimba ilifaulu kutoka ama kana kuna mashaka ya kuwepo kwa matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)

    Marejeo:

    Hauhitaji kufanya ultrasound baada ya kutoa mimba kutumia tembe. Ultrasound itahitajika tu ikiwa kuna mashaka ya matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)au ikiwa kuna mashaka kama mimba ilitoka. Kama utaendelea kuhisi dalili za mimba (ulaini wa matiti, kichefuchefu,uchovu n.k) baada ya kutumia tembe, utahitaji kushauriana na mhudumu wa afya kwa hatua za kufuata. Kuna uwezekano kuwa hatua inayofuata itakuwa uchunguzi wa ultrasound, kama itazingatiwa kufaa. Kwa taarifa zaidi, unaweza kuwasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi kujifunza zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Unaweza ukahitaji utaratibu wa upasuaji ikiwa bado una ujauzito baada ya kumeza tembe. Kumbuka! Matibabu ya uaviaji mimba usiyokamilika yanapatikana kwa urahisi popote duniani. Una haki kupata huduma hii, hata kama uaviaji mimba umebanwa kisheria katika nchi yako.

Utoaji mimba kwa matibabu na kuzaa baadaye

    Unaweza kupata tena ujauzito haraka hata baada ya siku 8 baada ya matibabu ya uaviaji mimba. Ikiwa utafanya ngono, unastahili kuzingatia kutumia mbinu za kupanga uzazi ili kuzuia mimba zisizotarajiwa.

    La, tembe za kuavya mimba hazisababishi kasoro za kuzaliwa katika mimba za siku za usoni.

    La, kuwa na uaviaji mimba kwa tembe haiwezi kuifanya vigumu kupata ujauzito katika siku za usoni.

Utoaji mimba kwa matibabu na kuzaa baadaye

    Unaweza kupata tena ujauzito haraka hata baada ya siku 8 baada ya matibabu ya uaviaji mimba. Ikiwa utafanya ngono, unastahili kuzingatia kutumia mbinu za kupanga uzazi ili kuzuia mimba zisizotarajiwa.

    La, tembe za kuavya mimba hazisababishi kasoro za kuzaliwa katika mimba za siku za usoni.

    La, kuwa na uaviaji mimba kwa tembe haiwezi kuifanya vigumu kupata ujauzito katika siku za usoni.

Maswali Mengine Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Mimba

    Ingawaje utoaji mimba ni kawaida, tunaweza kupata ugumu kuuzungumzia. Utoaji mimba bado umezungukwa na taarifa nyingi potofu, hadithi za uongo,na unyanyapaa. Ukizungumzia utoaji mimba, jaribu utumie taarifa za ukweli kutoka kwa vyanzo vya kuaminika, ukiepuka lugha ya unyanyapaa-watu tofauti hutoa mimba. Ingawa huenda haitakuwa rahisi, usianze ubishi. Badala yake, uliza maswali ya wazi kuhusu mtazamo na hisia za watu kuhusu utoaji mimba.

    Hali ya utoaji mimba kukubaliwa na sheria inategema ni wapi unapoishi. Katika nchi zingine, utoaji mimba imekubaliwa na sheria kwa wiki fulani ya mimba, ilhali katika nchi zingine utoaji mimba ni imekubaliwa chini ya sheria katika hali fulani (kwa mfano, kwa hali ya ubakaji ama hatari kwa maisha ya mtu aliye mjamzito). Tembe za utoaji mimba huwa zimekubaliwa na sheria katika nchi ambazo utoaji mimba imekubaliwa na sheria, ila haziwezi tumiwa nje ya kituo cha afya. Kuna nchi zingine ambamo utoaji mimba umepigwa marufuku. Jifunze zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Kila mtu hupitia mambo tofauti wakati wa utoaji mimba. Kuna wale watahisi kama wametulia na wana furaha, na kuna wale watahisi huzuni. Hisia zote ni kawaida. Hata hivyo, ni nadra kuwa na hisia hasi kwa muda mrefu.Kile kinachoweza kuathiri vibaya afya yako ya kiakili ni kukumbana na unyanyapaa na hukumu. Kumbuka kwamba hauko peke yako- utoaji mimba ni kitu cha kawaida. Usaidizi kutoka kwa marafiki, familia au mashirika ya mtaani unaweza kusaidia.

    Marejeo:

    Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

    Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za utoaji mimba kwa matibabu (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya wote kote duniani.

    Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba:

    1) Utoaji mimba kwa matibabu: Utoaji mimba kwa matibabu hutumia madawa ya famakolojia ili kutamatisha ujauzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.

    2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga ujauzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha ujauzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

Maswali Mengine Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Mimba

    Ingawaje utoaji mimba ni kawaida, tunaweza kupata ugumu kuuzungumzia. Utoaji mimba bado umezungukwa na taarifa nyingi potofu, hadithi za uongo,na unyanyapaa. Ukizungumzia utoaji mimba, jaribu utumie taarifa za ukweli kutoka kwa vyanzo vya kuaminika, ukiepuka lugha ya unyanyapaa-watu tofauti hutoa mimba. Ingawa huenda haitakuwa rahisi, usianze ubishi. Badala yake, uliza maswali ya wazi kuhusu mtazamo na hisia za watu kuhusu utoaji mimba.

    Hali ya utoaji mimba kukubaliwa na sheria inategema ni wapi unapoishi. Katika nchi zingine, utoaji mimba imekubaliwa na sheria kwa wiki fulani ya mimba, ilhali katika nchi zingine utoaji mimba ni imekubaliwa chini ya sheria katika hali fulani (kwa mfano, kwa hali ya ubakaji ama hatari kwa maisha ya mtu aliye mjamzito). Tembe za utoaji mimba huwa zimekubaliwa na sheria katika nchi ambazo utoaji mimba imekubaliwa na sheria, ila haziwezi tumiwa nje ya kituo cha afya. Kuna nchi zingine ambamo utoaji mimba umepigwa marufuku. Jifunze zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Kila mtu hupitia mambo tofauti wakati wa utoaji mimba. Kuna wale watahisi kama wametulia na wana furaha, na kuna wale watahisi huzuni. Hisia zote ni kawaida. Hata hivyo, ni nadra kuwa na hisia hasi kwa muda mrefu.Kile kinachoweza kuathiri vibaya afya yako ya kiakili ni kukumbana na unyanyapaa na hukumu. Kumbuka kwamba hauko peke yako- utoaji mimba ni kitu cha kawaida. Usaidizi kutoka kwa marafiki, familia au mashirika ya mtaani unaweza kusaidia.

    Marejeo:

    Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

    Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za utoaji mimba kwa matibabu (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya wote kote duniani.

    Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba:

    1) Utoaji mimba kwa matibabu: Utoaji mimba kwa matibabu hutumia madawa ya famakolojia ili kutamatisha ujauzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.

    2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga ujauzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha ujauzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

HowToUseAbortionPill.org inashirikiana na shirika lisilo la faida lililosajiliwa huko Amerika-501c (3)
HowToUseAbortionPill.org hutoa yaliyomo yaliyokusudiwa kwa sababu ya habari tu na haihusiani na shirika la matibabu.

Inaendeshwa na Women First Digital