Maswali kuhusu utoaji Mimba-Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Tembe za Kuavya Mimba

Nani Anaweza Kutumia Tembe za Kuavya Mimba?

    La, tumia idadi sawa ya tembe tunazopendekeza kwa kila mtu. Tafiti zinaonyesha kuwa ufanisi wa dawa haupungui kama una uzani zaidi . Hauhitaji kumeza kipimo tofauti au kumeza tembe Zaidi.

    Hauhitaji kubadili dozi au idadi ya tembe ikiwa umegundua kuwa una mimba ya mapacha. Maagizo ya kutumia tembe kwa mimba ya mapacha ni sawa na yale ya mimba ya mtoto mmoja.

    La, kila mimba ni tukio la kipekee. Ikiwa uliwahi kutumia tembe za kuavya mimba awali, hauhitaji kipimo zaidi ikiwa utaitumia tena kwa mimba tofauti isiyohitajika.

    Ikiwa umeweka kitanzi/lupu kwenye mfuko wako wa kizazi (kwa mfano IUD ya shaba au IUD yenye homoni ya progesterone) inapendekezwa itolewe kabla ya kutumia tembe za kutoa mimba.

    Unaweza kunyonyesha kama kawaida wakati wa kutoa mimba kwa tembe. Mifepristone na misoprostol zinaingia kwa maziwa ya mama kwa kiasi kidogo sana, ambacho hakiwezi kusababisha madhara yoyote au kumdhuru mtoto wako. Unaweza kuendelea kunyonyesha bila kukatiza wakati unatoa mimba kwa kutumia tembe.

    Ikiwa unaishi na VVU, unaweza kutoa mimba kwa kutumia tembe kama tu watu wengine. Unashauriwa kila mara kwamba uwe unatumia dawa za kupunguza makali ya VVU kwa afya bora zaidi.

    Iwapo una upungufu wa damu (una madini ya chuma pungufu kwenye damu) bado unaweza kutoa mimba kwa kutumia tembe, lakini ni bora kutambua mtoa huduma anayeweza kupatikana wa kukusaidia unapohitaji. Iwapo una upungufu wa damu uliokidhiri, ni bora zaidi kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia tembe za kuavya mimba.

    La, kutumia tembe za kuavya mimba mapema unapokuwa mja mzito ni salama hata kama ulijifungua kwa njia ya upasuaji.

    Hakuna uhusiano ambao umepatikana kati ya mifepristone na kasoro za kuzaliwa. Hata hivyo, misoprostol huwa inasababisha kiwango kidogo cha ongezeko za kasoro za kuzaliwa.Kama utameza misoprostol na bado ungali mja mzito baada ya kumeza tembe, unaweza kupoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa hautapoteza mimba hiyo na uwe nayo hadi wakati utimie, hatari ya kasoro za maumbile kwa mtoto zinazohusishwa na misoprostol bado huwa chini ya 10 kati ya 1000.

    Ikiwa ulifanyiwa ufungaji wa uzazi wa kike hapo awali na sasa una mimba, bado unaweza kutumia tembe za kutoa mimba. Hata hivyo, uko katika hatari ya juu zaidi kuliko mtu wa kawaida ya kuwa na ujauzito unaojitunga nje ya mji wa mimba, kwa sababu ufungaji wa uzazi huwacha kovu katika mirija ya uzazi. Unaweza kuchagua kuendelea kutumia tembe za kutoa mimba, hata hivyo, ikiwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, tembe hazitafanya kazi. Hazitakudhuru, lakini mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba itaendelea kukuwa na kukuweka katika hali ambayo inaweza kutishia maisha yako. Ikiwa ni mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, utahitaji huduma ya matibabu maalum. Ikiwa ulifanyiwa taratibu wa ufungaji wa uzazi awali na umefanya kipimo cha ultrasound na kikaonyesha kuwa mimba imejitunga ndani ya mji wa mimba, (sio nje ya mji wa mimba) ni salama kutumia tembe.

    Ikiwa ulikuwa na mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba hapo na ikatibiwa, na sasa una mimba, bado unaweza kutumia tembe za kutoa mimba. Hata hivyo, uko katika hatari ya juu zaidi kuliko mtu wa kawaida ya kuwa na ujauzito mwingine unaojitunga nje ya mji wa mimba. Unaweza kuchagua kuendelea kutumia tembe za kutoa mimba, hata hivyo, ikiwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, tembe hazitafanya kazi. Hazitakudhuru, lakini mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba itaendelea kukuwa na kukuweka katika hali ambayo inaweza kutishia maisha yako. Ikiwa ni mimba ingine iliyojitunga nje ya mji wa mimba, utahitaji huduma ya matibabu maalum. Ikiwa hapo awali ulikuwa na mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba na ulifanya kipimo cha ultrasound na kikaonyesha kuwa mimba imejitunga ndani ya mji wa mimba, (sio nje ya mji wa mimba) ni salama kutumia tembe.

    Mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba hugunduliwa na kipimo cha ultrasaound. Ikiwa imethibitishwa kuwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, haipendekezwi kutumia tembe za kutoa mimba kwasababu hazitafanya kazi. Badala yake, lazima utafute huduma ya matibabu kwa mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba kwa sababu hii sio mimba kamili. Hata katika nchi ambazo utoaji mimba si halali unaweza kupata utaratibu wa kisheria wa kutoa mimba hii.

    Kama mwanamume aliyebadili jinsia ama mtu asiyejitambulisha na jinsia yoyote, ni salama kutoa mimba kwa kutumia tembe. Kama unatumia homoni za kiume, misoprostol ama mifepristone haitaziharibu. Hizi tembe za utoaji mimba zinaweza kutumiwa salama kama unatumia homoni (GnRH) za kuwachilia testosterone (T) na/ama gonadotrophin. Hata hivyo, unaweza kukumbana na ugumu wa kupata utunzaji jumuishi wa utoaji mimba. Jifunze zaidi kuhusu utunzaji wa kutoa mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

Nani Anaweza Kutumia Tembe za Kuavya Mimba?

    La, tumia idadi sawa ya tembe tunazopendekeza kwa kila mtu. Tafiti zinaonyesha kuwa ufanisi wa dawa haupungui kama una uzani zaidi . Hauhitaji kumeza kipimo tofauti au kumeza tembe Zaidi.

    Hauhitaji kubadili dozi au idadi ya tembe ikiwa umegundua kuwa una mimba ya mapacha. Maagizo ya kutumia tembe kwa mimba ya mapacha ni sawa na yale ya mimba ya mtoto mmoja.

    La, kila mimba ni tukio la kipekee. Ikiwa uliwahi kutumia tembe za kuavya mimba awali, hauhitaji kipimo zaidi ikiwa utaitumia tena kwa mimba tofauti isiyohitajika.

    Ikiwa umeweka kitanzi/lupu kwenye mfuko wako wa kizazi (kwa mfano IUD ya shaba au IUD yenye homoni ya progesterone) inapendekezwa itolewe kabla ya kutumia tembe za kutoa mimba.

    Unaweza kunyonyesha kama kawaida wakati wa kutoa mimba kwa tembe. Mifepristone na misoprostol zinaingia kwa maziwa ya mama kwa kiasi kidogo sana, ambacho hakiwezi kusababisha madhara yoyote au kumdhuru mtoto wako. Unaweza kuendelea kunyonyesha bila kukatiza wakati unatoa mimba kwa kutumia tembe.

    Ikiwa unaishi na VVU, unaweza kutoa mimba kwa kutumia tembe kama tu watu wengine. Unashauriwa kila mara kwamba uwe unatumia dawa za kupunguza makali ya VVU kwa afya bora zaidi.

    Iwapo una upungufu wa damu (una madini ya chuma pungufu kwenye damu) bado unaweza kutoa mimba kwa kutumia tembe, lakini ni bora kutambua mtoa huduma anayeweza kupatikana wa kukusaidia unapohitaji. Iwapo una upungufu wa damu uliokidhiri, ni bora zaidi kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia tembe za kuavya mimba.

    La, kutumia tembe za kuavya mimba mapema unapokuwa mja mzito ni salama hata kama ulijifungua kwa njia ya upasuaji.

    Hakuna uhusiano ambao umepatikana kati ya mifepristone na kasoro za kuzaliwa. Hata hivyo, misoprostol huwa inasababisha kiwango kidogo cha ongezeko za kasoro za kuzaliwa.Kama utameza misoprostol na bado ungali mja mzito baada ya kumeza tembe, unaweza kupoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa hautapoteza mimba hiyo na uwe nayo hadi wakati utimie, hatari ya kasoro za maumbile kwa mtoto zinazohusishwa na misoprostol bado huwa chini ya 10 kati ya 1000.

    Ikiwa ulifanyiwa ufungaji wa uzazi wa kike hapo awali na sasa una mimba, bado unaweza kutumia tembe za kutoa mimba. Hata hivyo, uko katika hatari ya juu zaidi kuliko mtu wa kawaida ya kuwa na ujauzito unaojitunga nje ya mji wa mimba, kwa sababu ufungaji wa uzazi huwacha kovu katika mirija ya uzazi. Unaweza kuchagua kuendelea kutumia tembe za kutoa mimba, hata hivyo, ikiwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, tembe hazitafanya kazi. Hazitakudhuru, lakini mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba itaendelea kukuwa na kukuweka katika hali ambayo inaweza kutishia maisha yako. Ikiwa ni mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, utahitaji huduma ya matibabu maalum. Ikiwa ulifanyiwa taratibu wa ufungaji wa uzazi awali na umefanya kipimo cha ultrasound na kikaonyesha kuwa mimba imejitunga ndani ya mji wa mimba, (sio nje ya mji wa mimba) ni salama kutumia tembe.

    Ikiwa ulikuwa na mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba hapo na ikatibiwa, na sasa una mimba, bado unaweza kutumia tembe za kutoa mimba. Hata hivyo, uko katika hatari ya juu zaidi kuliko mtu wa kawaida ya kuwa na ujauzito mwingine unaojitunga nje ya mji wa mimba. Unaweza kuchagua kuendelea kutumia tembe za kutoa mimba, hata hivyo, ikiwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, tembe hazitafanya kazi. Hazitakudhuru, lakini mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba itaendelea kukuwa na kukuweka katika hali ambayo inaweza kutishia maisha yako. Ikiwa ni mimba ingine iliyojitunga nje ya mji wa mimba, utahitaji huduma ya matibabu maalum. Ikiwa hapo awali ulikuwa na mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba na ulifanya kipimo cha ultrasound na kikaonyesha kuwa mimba imejitunga ndani ya mji wa mimba, (sio nje ya mji wa mimba) ni salama kutumia tembe.

    Mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba hugunduliwa na kipimo cha ultrasaound. Ikiwa imethibitishwa kuwa una mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba, haipendekezwi kutumia tembe za kutoa mimba kwasababu hazitafanya kazi. Badala yake, lazima utafute huduma ya matibabu kwa mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba kwa sababu hii sio mimba kamili. Hata katika nchi ambazo utoaji mimba si halali unaweza kupata utaratibu wa kisheria wa kutoa mimba hii.

    Kama mwanamume aliyebadili jinsia ama mtu asiyejitambulisha na jinsia yoyote, ni salama kutoa mimba kwa kutumia tembe. Kama unatumia homoni za kiume, misoprostol ama mifepristone haitaziharibu. Hizi tembe za utoaji mimba zinaweza kutumiwa salama kama unatumia homoni (GnRH) za kuwachilia testosterone (T) na/ama gonadotrophin. Hata hivyo, unaweza kukumbana na ugumu wa kupata utunzaji jumuishi wa utoaji mimba. Jifunze zaidi kuhusu utunzaji wa kutoa mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

Aina za Tembe za Kuavya Mimba na Matumizi zao

    Utafiti unaonyesha kuwa utoaji mimba kwa matibabu inapendekezwa mara nyingo kwa mimba kabla ya wiki 13 tangu hedhi yako ya mwisho. Utaratibu wa HowToUseAbortionPill imetolewa kwa ajili ya mimba hadi wiki 13.Temeb za kutoa mimba zinaweza kutumika kwa mimba kubwa zaidi ya hio, lakini itahitaji taratibu na mazingatio tofauti kw usalama. Kwa taarifa zaidi, unaweza wasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi ili kujifunza zaidi kuhusu rasilimali za utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Utoaji mimba kwa tembe ni salama mno na una ufanisi sana ikitumiwa inavyofaa.Utoaji mimba kwa kutumia mifepristone na misoprostol hufaulu kwa zaidi ya asilimia 95, na uwezo wa matatizo kutokea huwa chini ya asilimia 1 kwa mimba ya hadi wiki 10 na asilimia 3 kwa mimba kati ya wiki 10 na 13.Ukitumia misoprostol pekee, utoaji mimba una kiwango cha kufaulu cha asilimia 80-85, na uwezo wa matatizo wa asilimia 1-4 kwa mimba ya hadi wiki 13. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, utoaji mimba kwa tembe unaweza kufanywa kwa usalama na ufanisi nyumbani, bora uwe na taarifa sahihi na unaweza kupata tembe zenye viwango bora.

    Marejeo:

    Kuna aina mbili ya tembe za kuavya mimba, na kila moja ina mbinu tofauti ya utenda kazi. Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa ujauzito, ilhali virutubishi vinavyotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa tumbo la uzazi (mwanya katika tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, na hivyo kusukuma ujauzito nje.

    Misoprostol husababisha tumbo la uzazi kujikaza na hivyo kutoa ujauzito.

    Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa mimba

    Ndio, unaweza kutumia misoprostol salama ukiwa nyumbani. Unapotumia tembe za misoprostol, jaribu kuhakikisha kuwa uko katika sehemu (kama kwako nyumbani) ambapo una ufaragha na unaweza kulala chini kwa saa chache baada ya kumeza tembe. Kuwa na mtu karibu nawe anayeweza kukuangalia na kukuletea chai moto au kitu cha kula inaweza kusaidia sana.

    Usinywe au kula kitu chochote kwa dakika 30 unaporuhusu misoprostol kuyeyuka. Baada ya dakika 30 kupita, unaweza kunywa maji ili kumeza mabaki ya tembe, na kwa jumla kiasi cha maji unachostahili ili kuhisi mwili una maji ya kutosha.

    Ndio, unaweza kunywa maji kukusaidia kumeza mifepristone.

    Kuna njia mbili za kutumia misoprostol na ufaulu: kuweka tembe ndani ya uke (kwenye uke) au chini ya ulimi wako (kupitia mdomo). HowToUseAbortionPill inapendekeza kwamba utumie misoprostol tu chini ya ulimi wako kwa sababu tembe huyeyuka haraka, na ni ya faragha zaidi kwa sababu haziachi mabaki yanayoonekana katika mwili wako.

    Kutumia mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol na kutumia misoprostol-pekee yote ni machaguo bora. Hata hivyo, ikiwa inapatikana na ni ya bei nafuu kwako, mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol unapaswa kuwa chaguo lako kwani ni bora kidogo kuliko misoprostol pekee.

    Wanawake 98 kati ya 100 huwa na uaviaji mimba kamili ikiwa mifepristone na misoprostol zimetumika kwa pamoja. Takriban wanawake 95 kati ya 100 watakuwa na uaviaji mimba kamili ikiwa misoprostol pekee inatumika.

    Mifepristone na misoprostol hutumika pamoja kwa sababu tembe hizi hukamilishana. Mifepristone huzuia mimba kumea.Dawa inayotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa uzazi (kufungua tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, hivyo kusukuma nje ujauzito.

    Ikiwa utatumia tembe za misoprostol chini ya ulimi wako, hakuna mtu anaweza kujua kuwa ulitumia tembe za kuavya mimba kwa sababu utameza kila kitu baada ya dakika 30. Ikiwa mtu atauliza, unaweza kusema ulipoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa utatumia misoprostol kupitia uke, koti ya tembe huenda isiyeyuke kabisa kwa siku moja au mbili. Ikiwa unahitaji kutafuta usaidizi wa kiafya wa dharura kati ya saa 48 kwa sababu ulitumia misoprostol kupitia uke, mhudumu wa afya anaweza kuona koti nyeupe za tembe katika uke wako. Hii ndio maana HowToUseAbortionPill hupendekeza kutumia misoprostol chini ya ulimi wako na si ndani ya uke wako.

    Kama una mzio wa dawa za NSAID (ikiwemo ibuprofen), acetaminophen (Tylenol/Paracetamol) inapendekezwa kama dawa mbadala. Inapatikana katika duka za dawa katika nchi nyingi.Tumia tembe 2 (tembe za miligramu 325) kila saa 4-6 inavyohitajika kwa maumivu. Dozi ya juu sana katika saa 24 ni miligramu 400.

    Marejeo:

Aina za Tembe za Kuavya Mimba na Matumizi zao

    Utafiti unaonyesha kuwa utoaji mimba kwa matibabu inapendekezwa mara nyingo kwa mimba kabla ya wiki 13 tangu hedhi yako ya mwisho. Utaratibu wa HowToUseAbortionPill imetolewa kwa ajili ya mimba hadi wiki 13.Temeb za kutoa mimba zinaweza kutumika kwa mimba kubwa zaidi ya hio, lakini itahitaji taratibu na mazingatio tofauti kw usalama. Kwa taarifa zaidi, unaweza wasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi ili kujifunza zaidi kuhusu rasilimali za utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Utoaji mimba kwa tembe ni salama mno na una ufanisi sana ikitumiwa inavyofaa.Utoaji mimba kwa kutumia mifepristone na misoprostol hufaulu kwa zaidi ya asilimia 95, na uwezo wa matatizo kutokea huwa chini ya asilimia 1 kwa mimba ya hadi wiki 10 na asilimia 3 kwa mimba kati ya wiki 10 na 13.Ukitumia misoprostol pekee, utoaji mimba una kiwango cha kufaulu cha asilimia 80-85, na uwezo wa matatizo wa asilimia 1-4 kwa mimba ya hadi wiki 13. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, utoaji mimba kwa tembe unaweza kufanywa kwa usalama na ufanisi nyumbani, bora uwe na taarifa sahihi na unaweza kupata tembe zenye viwango bora.

    Marejeo:

    Kuna aina mbili ya tembe za kuavya mimba, na kila moja ina mbinu tofauti ya utenda kazi. Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa ujauzito, ilhali virutubishi vinavyotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa tumbo la uzazi (mwanya katika tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, na hivyo kusukuma ujauzito nje.

    Misoprostol husababisha tumbo la uzazi kujikaza na hivyo kutoa ujauzito.

    Mifepristone huzuia homoni zinazohitajika kwa ukuaji wa mimba

    Ndio, unaweza kutumia misoprostol salama ukiwa nyumbani. Unapotumia tembe za misoprostol, jaribu kuhakikisha kuwa uko katika sehemu (kama kwako nyumbani) ambapo una ufaragha na unaweza kulala chini kwa saa chache baada ya kumeza tembe. Kuwa na mtu karibu nawe anayeweza kukuangalia na kukuletea chai moto au kitu cha kula inaweza kusaidia sana.

    Usinywe au kula kitu chochote kwa dakika 30 unaporuhusu misoprostol kuyeyuka. Baada ya dakika 30 kupita, unaweza kunywa maji ili kumeza mabaki ya tembe, na kwa jumla kiasi cha maji unachostahili ili kuhisi mwili una maji ya kutosha.

    Ndio, unaweza kunywa maji kukusaidia kumeza mifepristone.

    Kuna njia mbili za kutumia misoprostol na ufaulu: kuweka tembe ndani ya uke (kwenye uke) au chini ya ulimi wako (kupitia mdomo). HowToUseAbortionPill inapendekeza kwamba utumie misoprostol tu chini ya ulimi wako kwa sababu tembe huyeyuka haraka, na ni ya faragha zaidi kwa sababu haziachi mabaki yanayoonekana katika mwili wako.

    Kutumia mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol na kutumia misoprostol-pekee yote ni machaguo bora. Hata hivyo, ikiwa inapatikana na ni ya bei nafuu kwako, mchanganyiko wa mifepristone na misoprostol unapaswa kuwa chaguo lako kwani ni bora kidogo kuliko misoprostol pekee.

    Wanawake 98 kati ya 100 huwa na uaviaji mimba kamili ikiwa mifepristone na misoprostol zimetumika kwa pamoja. Takriban wanawake 95 kati ya 100 watakuwa na uaviaji mimba kamili ikiwa misoprostol pekee inatumika.

    Mifepristone na misoprostol hutumika pamoja kwa sababu tembe hizi hukamilishana. Mifepristone huzuia mimba kumea.Dawa inayotumika katika misoprostol hufanya kazi kwa kulegeza na kufungua mlango wa uzazi (kufungua tumbo la uzazi) na kusababisha tumbo la uzazi kujikaza, hivyo kusukuma nje ujauzito.

    Ikiwa utatumia tembe za misoprostol chini ya ulimi wako, hakuna mtu anaweza kujua kuwa ulitumia tembe za kuavya mimba kwa sababu utameza kila kitu baada ya dakika 30. Ikiwa mtu atauliza, unaweza kusema ulipoteza mimba kwa njia ya kawaida. Ikiwa utatumia misoprostol kupitia uke, koti ya tembe huenda isiyeyuke kabisa kwa siku moja au mbili. Ikiwa unahitaji kutafuta usaidizi wa kiafya wa dharura kati ya saa 48 kwa sababu ulitumia misoprostol kupitia uke, mhudumu wa afya anaweza kuona koti nyeupe za tembe katika uke wako. Hii ndio maana HowToUseAbortionPill hupendekeza kutumia misoprostol chini ya ulimi wako na si ndani ya uke wako.

    Kama una mzio wa dawa za NSAID (ikiwemo ibuprofen), acetaminophen (Tylenol/Paracetamol) inapendekezwa kama dawa mbadala. Inapatikana katika duka za dawa katika nchi nyingi.Tumia tembe 2 (tembe za miligramu 325) kila saa 4-6 inavyohitajika kwa maumivu. Dozi ya juu sana katika saa 24 ni miligramu 400.

    Marejeo:

Hali ambayo matumizi ya tembe ya uavyaji mimba hayafai

    Unapaswa kuepuka kutumia tembe za kuavya mimba nyumbani kwa kufuata itifaki ya HowToUseAbortionPill ikiwa una mimba zaidi ya wiki 13 (siku 91); ikiwa una mzio wa mifepristone au misoprostol; ikiwa una matatizo makubwa ya afya, ikijumuisha matatizo ya kuganda kwa damu; au ikiwa unaamini au unajua kuwa mimba inakua nje ya mji wa mimba (mimba nje ya tumbo ya uzazi).

Hali ambayo matumizi ya tembe ya uavyaji mimba hayafai

    Unapaswa kuepuka kutumia tembe za kuavya mimba nyumbani kwa kufuata itifaki ya HowToUseAbortionPill ikiwa una mimba zaidi ya wiki 13 (siku 91); ikiwa una mzio wa mifepristone au misoprostol; ikiwa una matatizo makubwa ya afya, ikijumuisha matatizo ya kuganda kwa damu; au ikiwa unaamini au unajua kuwa mimba inakua nje ya mji wa mimba (mimba nje ya tumbo ya uzazi).

Madhara na Matatizo ya Tembe za Kuavya Mimba

    Kila utoaji mimba huwa tofauti. Unaweza kupata maumivi makali zaidi na kutokwa damu nyingi zaidi kushinda hedhi ya kawaida (ikiwa wewe huumwa wakati wa hedhi). Lakini pia ni kawaida kama utapata maumivu yasiyo makali na damu itoke tu kama vile hedhi ya kawaida. Madhara mengine ya kawaida ni kichefuchefu, kuhara,homa, na maumivu ya kichwa. Hata hivyo, unapaswa kuhisi nafuu chini ya saa 24. Ukianza kuhisi mgonjwa zaidi, basi tafuta msaada wa kimatabibu.

    Marejeo:

    Kwa baadhi ya watu, maumivu ya tumbo huwa makali- zaidi ya maumivu ya hedhi (ikiwa huwa unapata maumivu ya hedhi) na umwagikaji damu huwa zaidi ya ule wa hedhi. Unaweza kutokwa na madonge ya damu hadi ukubwa wa limau katika saa za kwanza baada ya kumeza misoprostol. Kwa wengine, maumivu huwa hafifu na umwagikaji wa damu huwa kama hedhi ya kawaida. Umwagikaji wa damu kwa jumla huwa nzito zaidi ndani ya saa 24 za kwanza baada ya kutumia misoprostol.

    Ili tembe ya kutoa mimba ifanye kazi, lazima utokwe damu. Tafuta msaada wa kiafya ikiwa hauna umwagikaji wa damu au una umwagikaji mdogo wa damu unaofuatwa na maumivu makali (hasa katika bega la kulia) ambayo hayapunguzwi na ibuprofen. Hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito ulio nje ya tumbo la uzazi (mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba). Ingawa ni nadra, inaweza kuwa tishio la maisha. Unaweza pia kuwasiliana na marafiki zetu katika www.safe2choose.org ili kuongea na mshauri wa uaviaji mimba aliye na mafunzo ikiwa unahisi kuwa uaviaji mimba haukufanikiwa.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa unalowesha visodo viwili vya hedhi kila saa kwa saa 2 mfululizo baada ya kufikiri ujauzito ushatoka. Kulowa kunamaanisha kuwa kisodo cha hedhi kimejaa damu mbele – hadi – nyuma, upande- hadi – upande na juu- hadi – chini.

    Meza tembe 3-4 (200 mg) za ibuprofen baada ya kila saa 6-8 ili kusaidia kuondoa maumivu yako. Kumbuka kuwa unaweza kumeza ibuprofen kabla ya kutumia misoprostol, pia

    Baada ya misoprostol kuyeyuka kwa dakika 30, unaweza kula unavyotaka. Hakuna vikwazo kwa aina ya vyakula unavyoweza kukula. HowToUseAbortionPill inapendekeza vyakula rahisi, vilivyokauka (kama vile kraka au tosti) kwa sababu vinaweza kusaidia kichefuchefu, ilhali mboga za kijani kibichi, mayai na nyama nyekundu inaweza kurejesha madini yaliyopotea wakati wa kuavya mimba.

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kunywa kinywaji chochote unachokipenda (isipokuwa pombe).

    HowToUseAbortionPill inapendekeza uepuke pombe wakati wa mchakato wa utoaji mimba ili kupunguza athari hasi ya pombe kwa dawa na uwezo wako wa kujitunza. Pombe inaweza kuathiri umwagikaji wa damu. Mara una hakika kuwa uaviaji mimba umefaulu ni sawa kukunywa pombe.

    Kwa wengi ujauzito utatoka na wahisi maumivu na umwagikaji damu mbaya zaidi baada ya saa 4-5 ya kutumia dozi ya kwanza ya misoprostol. Watu wengi wataanza kuhisi vyema chini ya saa 24 baada ya kutumia dozi ya mwisho ya misoprostol. Ni kawaida kuendelea kuona umwagikaji mdogo wa damu na madoadoa hadi hedhi yako inayofuata takriban wiki 3-4.

    Baada ya kutumia misoprostol, ni kawaida kuhisi kuwa mgonjwa kwa tumbo lako, kuhara, kibaridi, au hata kuhisi una joto katika kipindi hiki. Wengi wanaripoti kuwa wanajua wakati mimba imetoka kwa sababu umwagikaji wa damu unapungua,madhara ya dawa yanapungua, na dalili za mimba zinaanza kupungua.

    Matatizo katika utoaji mimba kwa matibabu ni nadra kabisa. Hata hivyo, ni muhimu uwe na uwezo wa kutambua dalili za matatizio. Kama utatokwa na damu nyingi (kulowesha taulo 2 za kawaida za hedhi kila saa moja kwa saa 2 mfululizo), una maumivu makali ambayo hayapungui baada ya kumeza ibuprofen au unaaza kujihisi mgonjwa siku yoyote baada ya kutumia misoprostol, unapaswa kutafuta ushauri wa kimatimabu.

    Je utoaji mimba kwa matibabu ama utoaji mimba nyumbani unakubaliwa na sheria katika nchi yako? Huenda utahitajika kuwa mwangalifu kuhusu kile utakachosema. Utoaji mimba kwa matibabu una dalilil sawa kama mimba kuharibika yenyewe ( pia inayojulikana kama mimba kutoka kwa hiari). Kwa hivyo, unaweza kusema vitu kama ‘natokwa damu,lakini sihisi kama ni hedhi yangu ya kawaida”

    Marejeo:

    Kuna njia tofauti za kujua kama utoaji mimba ulifaulu. Wakati wa utoaji mimba, unaweza kujua kama ulifikia vijinyama vya mimba ( vitafanana kama vile zabibu ndogo nyeusi kidogo na utando mwembamba au kifuko kidogo kilichozungukwa na utando mlaini mweupe) Hii ni ishara kuwa utoaji mimba ulifaulu. Hata hivyo, huenda haitakuwa rahisi kutambua vijinyama vya mimba. Ishara ingine ya utoaji mimba uliofaulu ni kupotea kwa dalili za mimba, kama vile ulaini wa matiti na kichefuchefu

    Kufanya kipimo cha mimba nyumbani pia ni njia ingine ya kuthibiti kufaulu kwa utoaji mimba. Hata hivyo, fahamu kwamba kipimo kinaweza kuonyesha mimba iko wiki 4 baada ya utoaji mimba, kwa sababu ya mabaki ya homoni mwilini mwako. Uchunguzi wa ultrasound utahitajika tu kama kuna mashaka ikiwa mimba ilifaulu kutoka ama kana kuna mashaka ya kuwepo kwa matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)

    Marejeo:

    Hauhitaji kufanya ultrasound baada ya kutoa mimba kutumia tembe. Ultrasound itahitajika tu ikiwa kuna mashaka ya matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)au ikiwa kuna mashaka kama mimba ilitoka. Kama utaendelea kuhisi dalili za mimba (ulaini wa matiti, kichefuchefu,uchovu n.k) baada ya kutumia tembe, utahitaji kushauriana na mhudumu wa afya kwa hatua za kufuata. Kuna uwezekano kuwa hatua inayofuata itakuwa uchunguzi wa ultrasound, kama itazingatiwa kufaa. Kwa taarifa zaidi, unaweza kuwasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi kujifunza zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Ikiwa haukutokwa damu au kuhisi maumivu baada ya kutumia tembe, na unadhani bado una mimba, au umethibitisha kwa kipimo cha ultrasound kwaba mimba yako bado inamea, unaweza kurudia taratibu ya HowToUseAbortionPill hadi mimba ifike wiki 13.

    Ikiwa utathibitisha kuwa ujauzito wako umeacha kukua kwa kupitia kipimo cha ultrasound, lakini mimba haijatolewa kutoka kwa mji wa mimba,hio ni utoaji mimba usio kamilika (sawa na kuharibika kwa mimba) na unaweza kufanyiwa utaratibu wa upasuaji ili kuondoa mimba. Hii inapatikana kwa wingi kote duniani kwa sababu mimba yako haichukuliwi tena kuwa hai. Vinginevyo, ni salama kurudia mchakato wa utoaji mimba kwa tembe na kuna uwezekano utafanikiwa kutoa mimba hio kwa mchakato huo wa pili.

Madhara na Matatizo ya Tembe za Kuavya Mimba

    Kila utoaji mimba huwa tofauti. Unaweza kupata maumivi makali zaidi na kutokwa damu nyingi zaidi kushinda hedhi ya kawaida (ikiwa wewe huumwa wakati wa hedhi). Lakini pia ni kawaida kama utapata maumivu yasiyo makali na damu itoke tu kama vile hedhi ya kawaida. Madhara mengine ya kawaida ni kichefuchefu, kuhara,homa, na maumivu ya kichwa. Hata hivyo, unapaswa kuhisi nafuu chini ya saa 24. Ukianza kuhisi mgonjwa zaidi, basi tafuta msaada wa kimatabibu.

    Marejeo:

    Kwa baadhi ya watu, maumivu ya tumbo huwa makali- zaidi ya maumivu ya hedhi (ikiwa huwa unapata maumivu ya hedhi) na umwagikaji damu huwa zaidi ya ule wa hedhi. Unaweza kutokwa na madonge ya damu hadi ukubwa wa limau katika saa za kwanza baada ya kumeza misoprostol. Kwa wengine, maumivu huwa hafifu na umwagikaji wa damu huwa kama hedhi ya kawaida. Umwagikaji wa damu kwa jumla huwa nzito zaidi ndani ya saa 24 za kwanza baada ya kutumia misoprostol.

    Ili tembe ya kutoa mimba ifanye kazi, lazima utokwe damu. Tafuta msaada wa kiafya ikiwa hauna umwagikaji wa damu au una umwagikaji mdogo wa damu unaofuatwa na maumivu makali (hasa katika bega la kulia) ambayo hayapunguzwi na ibuprofen. Hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito ulio nje ya tumbo la uzazi (mimba iliyojitunga nje ya mji wa mimba). Ingawa ni nadra, inaweza kuwa tishio la maisha. Unaweza pia kuwasiliana na marafiki zetu katika www.safe2choose.org ili kuongea na mshauri wa uaviaji mimba aliye na mafunzo ikiwa unahisi kuwa uaviaji mimba haukufanikiwa.

    Tafuta msaada wa kiafya ikiwa unalowesha visodo viwili vya hedhi kila saa kwa saa 2 mfululizo baada ya kufikiri ujauzito ushatoka. Kulowa kunamaanisha kuwa kisodo cha hedhi kimejaa damu mbele – hadi – nyuma, upande- hadi – upande na juu- hadi – chini.

    Meza tembe 3-4 (200 mg) za ibuprofen baada ya kila saa 6-8 ili kusaidia kuondoa maumivu yako. Kumbuka kuwa unaweza kumeza ibuprofen kabla ya kutumia misoprostol, pia

    Baada ya misoprostol kuyeyuka kwa dakika 30, unaweza kula unavyotaka. Hakuna vikwazo kwa aina ya vyakula unavyoweza kukula. HowToUseAbortionPill inapendekeza vyakula rahisi, vilivyokauka (kama vile kraka au tosti) kwa sababu vinaweza kusaidia kichefuchefu, ilhali mboga za kijani kibichi, mayai na nyama nyekundu inaweza kurejesha madini yaliyopotea wakati wa kuavya mimba.

    Baada ya misoprostol kuyeyuka, unaweza kunywa kinywaji chochote unachokipenda (isipokuwa pombe).

    HowToUseAbortionPill inapendekeza uepuke pombe wakati wa mchakato wa utoaji mimba ili kupunguza athari hasi ya pombe kwa dawa na uwezo wako wa kujitunza. Pombe inaweza kuathiri umwagikaji wa damu. Mara una hakika kuwa uaviaji mimba umefaulu ni sawa kukunywa pombe.

    Kwa wengi ujauzito utatoka na wahisi maumivu na umwagikaji damu mbaya zaidi baada ya saa 4-5 ya kutumia dozi ya kwanza ya misoprostol. Watu wengi wataanza kuhisi vyema chini ya saa 24 baada ya kutumia dozi ya mwisho ya misoprostol. Ni kawaida kuendelea kuona umwagikaji mdogo wa damu na madoadoa hadi hedhi yako inayofuata takriban wiki 3-4.

    Baada ya kutumia misoprostol, ni kawaida kuhisi kuwa mgonjwa kwa tumbo lako, kuhara, kibaridi, au hata kuhisi una joto katika kipindi hiki. Wengi wanaripoti kuwa wanajua wakati mimba imetoka kwa sababu umwagikaji wa damu unapungua,madhara ya dawa yanapungua, na dalili za mimba zinaanza kupungua.

    Matatizo katika utoaji mimba kwa matibabu ni nadra kabisa. Hata hivyo, ni muhimu uwe na uwezo wa kutambua dalili za matatizio. Kama utatokwa na damu nyingi (kulowesha taulo 2 za kawaida za hedhi kila saa moja kwa saa 2 mfululizo), una maumivu makali ambayo hayapungui baada ya kumeza ibuprofen au unaaza kujihisi mgonjwa siku yoyote baada ya kutumia misoprostol, unapaswa kutafuta ushauri wa kimatimabu.

    Je utoaji mimba kwa matibabu ama utoaji mimba nyumbani unakubaliwa na sheria katika nchi yako? Huenda utahitajika kuwa mwangalifu kuhusu kile utakachosema. Utoaji mimba kwa matibabu una dalilil sawa kama mimba kuharibika yenyewe ( pia inayojulikana kama mimba kutoka kwa hiari). Kwa hivyo, unaweza kusema vitu kama ‘natokwa damu,lakini sihisi kama ni hedhi yangu ya kawaida”

    Marejeo:

    Kuna njia tofauti za kujua kama utoaji mimba ulifaulu. Wakati wa utoaji mimba, unaweza kujua kama ulifikia vijinyama vya mimba ( vitafanana kama vile zabibu ndogo nyeusi kidogo na utando mwembamba au kifuko kidogo kilichozungukwa na utando mlaini mweupe) Hii ni ishara kuwa utoaji mimba ulifaulu. Hata hivyo, huenda haitakuwa rahisi kutambua vijinyama vya mimba. Ishara ingine ya utoaji mimba uliofaulu ni kupotea kwa dalili za mimba, kama vile ulaini wa matiti na kichefuchefu

    Kufanya kipimo cha mimba nyumbani pia ni njia ingine ya kuthibiti kufaulu kwa utoaji mimba. Hata hivyo, fahamu kwamba kipimo kinaweza kuonyesha mimba iko wiki 4 baada ya utoaji mimba, kwa sababu ya mabaki ya homoni mwilini mwako. Uchunguzi wa ultrasound utahitajika tu kama kuna mashaka ikiwa mimba ilifaulu kutoka ama kana kuna mashaka ya kuwepo kwa matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)

    Marejeo:

    Hauhitaji kufanya ultrasound baada ya kutoa mimba kutumia tembe. Ultrasound itahitajika tu ikiwa kuna mashaka ya matatizo (kutokwa damu nyingi ama maambukizi)au ikiwa kuna mashaka kama mimba ilitoka. Kama utaendelea kuhisi dalili za mimba (ulaini wa matiti, kichefuchefu,uchovu n.k) baada ya kutumia tembe, utahitaji kushauriana na mhudumu wa afya kwa hatua za kufuata. Kuna uwezekano kuwa hatua inayofuata itakuwa uchunguzi wa ultrasound, kama itazingatiwa kufaa. Kwa taarifa zaidi, unaweza kuwasiliana na marafiki wetu kwenye www.womenonweb.org. Au enda kwenye ukurasa wa wasifu wa nchi kujifunza zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Marejeo:

    Ikiwa haukutokwa damu au kuhisi maumivu baada ya kutumia tembe, na unadhani bado una mimba, au umethibitisha kwa kipimo cha ultrasound kwaba mimba yako bado inamea, unaweza kurudia taratibu ya HowToUseAbortionPill hadi mimba ifike wiki 13.

    Ikiwa utathibitisha kuwa ujauzito wako umeacha kukua kwa kupitia kipimo cha ultrasound, lakini mimba haijatolewa kutoka kwa mji wa mimba,hio ni utoaji mimba usio kamilika (sawa na kuharibika kwa mimba) na unaweza kufanyiwa utaratibu wa upasuaji ili kuondoa mimba. Hii inapatikana kwa wingi kote duniani kwa sababu mimba yako haichukuliwi tena kuwa hai. Vinginevyo, ni salama kurudia mchakato wa utoaji mimba kwa tembe na kuna uwezekano utafanikiwa kutoa mimba hio kwa mchakato huo wa pili.

Utoaji mimba kwa matibabu na kuzaa baadaye

    Unaweza kupata tena ujauzito haraka hata baada ya siku 8 baada ya kutoa mimba kwa matibabu. Ikiwa utafanya ngono na hautaki kushika mimba, unastahili kuzingatia kutumia mbinu za kuzuia mimba ili kuzuia mimba zisizotarajiwa.

    La, tembe za kuavya mimba hazisababishi kasoro za kuzaliwa katika mimba za siku za usoni.

    La, kuwa na uaviaji mimba kwa tembe haiwezi kuifanya vigumu kupata ujauzito katika siku za usoni.

Utoaji mimba kwa matibabu na kuzaa baadaye

    Unaweza kupata tena ujauzito haraka hata baada ya siku 8 baada ya kutoa mimba kwa matibabu. Ikiwa utafanya ngono na hautaki kushika mimba, unastahili kuzingatia kutumia mbinu za kuzuia mimba ili kuzuia mimba zisizotarajiwa.

    La, tembe za kuavya mimba hazisababishi kasoro za kuzaliwa katika mimba za siku za usoni.

    La, kuwa na uaviaji mimba kwa tembe haiwezi kuifanya vigumu kupata ujauzito katika siku za usoni.

Maswali Mengine Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Mimba

    Ingawaje utoaji mimba ni kawaida, tunaweza kupata ugumu kuuzungumzia. Utoaji mimba bado umezungukwa na taarifa nyingi potofu, hadithi za uongo,na unyanyapaa. Ukizungumzia utoaji mimba, jaribu utumie taarifa za ukweli kutoka kwa vyanzo vya kuaminika, ukiepuka lugha ya unyanyapaa-watu tofauti hutoa mimba. Ingawa huenda haitakuwa rahisi, usianze ubishi. Badala yake, uliza maswali ya wazi kuhusu mtazamo na hisia za watu kuhusu utoaji mimba.

    Hali ya utoaji mimba kukubaliwa na sheria inategema ni wapi unapoishi. Katika nchi zingine, utoaji mimba imekubaliwa na sheria kwa wiki fulani ya mimba, ilhali katika nchi zingine utoaji mimba ni imekubaliwa chini ya sheria katika hali fulani (kwa mfano, kwa hali ya ubakaji ama hatari kwa maisha ya mtu aliye mjamzito). Tembe za utoaji mimba huwa zimekubaliwa na sheria katika nchi ambazo utoaji mimba imekubaliwa na sheria, ila haziwezi tumiwa nje ya kituo cha afya. Kuna nchi zingine ambamo utoaji mimba umepigwa marufuku. Jifunze zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Kila mtu hupitia mambo tofauti wakati wa utoaji mimba. Kuna wale watahisi kama wametulia na wana furaha, na kuna wale watahisi huzuni. Hisia zote ni kawaida. Hata hivyo, ni nadra kuwa na hisia hasi kwa muda mrefu.Kile kinachoweza kuathiri vibaya afya yako ya kiakili ni kukumbana na unyanyapaa na hukumu. Kumbuka kwamba hauko peke yako- utoaji mimba ni kitu cha kawaida. Usaidizi kutoka kwa marafiki, familia au mashirika ya mtaani unaweza kusaidia.

    Marejeo:

    Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

    Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za utoaji mimba kwa matibabu (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya wote kote duniani.

    Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba:

    1) Utoaji mimba kwa matibabu: Utoaji mimba kwa matibabu hutumia madawa ya famakolojia ili kutamatisha ujauzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.

    2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga ujauzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha ujauzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

Maswali Mengine Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Mimba

    Ingawaje utoaji mimba ni kawaida, tunaweza kupata ugumu kuuzungumzia. Utoaji mimba bado umezungukwa na taarifa nyingi potofu, hadithi za uongo,na unyanyapaa. Ukizungumzia utoaji mimba, jaribu utumie taarifa za ukweli kutoka kwa vyanzo vya kuaminika, ukiepuka lugha ya unyanyapaa-watu tofauti hutoa mimba. Ingawa huenda haitakuwa rahisi, usianze ubishi. Badala yake, uliza maswali ya wazi kuhusu mtazamo na hisia za watu kuhusu utoaji mimba.

    Hali ya utoaji mimba kukubaliwa na sheria inategema ni wapi unapoishi. Katika nchi zingine, utoaji mimba imekubaliwa na sheria kwa wiki fulani ya mimba, ilhali katika nchi zingine utoaji mimba ni imekubaliwa chini ya sheria katika hali fulani (kwa mfano, kwa hali ya ubakaji ama hatari kwa maisha ya mtu aliye mjamzito). Tembe za utoaji mimba huwa zimekubaliwa na sheria katika nchi ambazo utoaji mimba imekubaliwa na sheria, ila haziwezi tumiwa nje ya kituo cha afya. Kuna nchi zingine ambamo utoaji mimba umepigwa marufuku. Jifunze zaidi kuhusu utoaji mimba katika nchi yako.

    Kila mtu hupitia mambo tofauti wakati wa utoaji mimba. Kuna wale watahisi kama wametulia na wana furaha, na kuna wale watahisi huzuni. Hisia zote ni kawaida. Hata hivyo, ni nadra kuwa na hisia hasi kwa muda mrefu.Kile kinachoweza kuathiri vibaya afya yako ya kiakili ni kukumbana na unyanyapaa na hukumu. Kumbuka kwamba hauko peke yako- utoaji mimba ni kitu cha kawaida. Usaidizi kutoka kwa marafiki, familia au mashirika ya mtaani unaweza kusaidia.

    Marejeo:

    Mbinu za uaviaji mimba hazistahili kuchanganyishwa na mbinu za kuzuia mimba (mbinu za kupanga uzazi, ikijumuishwa na upangaji uzazi wa dharura). Mbinu za kupanga uzazi hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. Mbinu za kupanga uzazi, ikijumuisha upangaji uzazi wa dharura, haziwezi kutumika kutamatisha au kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. Unaweza kutembelea www.findmymethod.org ili kujifunza mengi kuhusu mbinu za kupanga uzazi.

    Tembe za upangaji uzazi wa dharura (ECPs) ni salama na njia faafu za kuzuia mimba baada ya kujamiiana bila kinga. Hufanya kazi kwa kuzuia kupevuka kwa yai (kuachiliwa kwa yai) au kwa kuzuia yai na mbegu za kiume kukutana. ECPs haziwezi kutamatisha ama kuhitilafiana na mimba iliyotungwa. ECPs ni tofauti na taratibu za utoaji mimba kwa matibabu (ambazo hujumuisha mifepristone na misoprostol). Matibabu haya yana manufaa ya pekee kwa afya ya wote kote duniani.

    Kuna njia mbili zitumikazo sana katika mbinu za uaviaji mimba:

    1) Utoaji mimba kwa matibabu: Utoaji mimba kwa matibabu hutumia madawa ya famakolojia ili kutamatisha ujauzito. Wakati mwingine dhana “ uaviaji mimba pasi upasuaji” au uaviaji mimba kwa tembe” pia huwa zinatumika.

    2) Uaviaji mimba kwa upasuaji: Katika taratibu za uaviaji mimba kwa upasuaji, mtaalamu aliyehitimu atamwaga ujauzito kutoka kwa tumbo la uzazi kupitia mlango wa uzazi ili kutamatisha ujauzito. Taratibu hizi hujumuisha ufyonzaji ombwe usiootomatiki (MVA) na upanuzi na uondoaji (D&E).

HowToUseAbortionPill.org inashirikiana na shirika lisilo la faida lililosajiliwa huko Amerika-501c (3)
HowToUseAbortionPill.org hutoa yaliyomo yaliyokusudiwa kwa sababu ya habari tu na haihusiani na shirika la matibabu.

Inaendeshwa na Women First Digital