Kabla ya kutumia tembe

Hakikisha unajisikia vizuri kabisa na umejiandaa kabla hujatoa mimba kwa kutumia vidonge.

1. Mimba kikokotoleo (calculator)
2. Vya Kuzingatia
3. Ushauri Wa Jumla
4. Kutengeneza mpango wa usalama
Pregnacy calculator

Mimba kikokotoleo (calculator)

Ujauzito wako ni wa muda gani? Utafiti unaonyesha kuwa mara nyingi utoaji mimba kwa kutumia vidonge unapendekezwa kwa mimba zenye umri chini ya wiki 13. Tumia kikokotoleo (calculator) hiki kujua ujauzito una muda gani?

Ikiwa kipindi chako cha mwisho kilianza tarehe au baadaye:

24 Februari 2023

Bado unaweza kuzingatia utumiaji wa kidonge cha kutoa mimba

Vya Kuzingatia

Wakati unaposumbuliwa na IUD (KITANZI)

Wakati ambapo unaishi na VVU

Kama unajali faragha yako

Wakati unaponyonyesha

Wakati unaposumbuliwa na upungufu wa damu

Ushauri Wa Jumla

Kula chakula kidogo (kwa mfano vyakula vikavu au vya kukausha inaweza kukusaidia usipate kichefuchefu)
Kunywa maji mengi kipindi chote cha mchakato huu
Wakati matumizi ya tembe za misoprostol,hakikisha uko kwenye eneo ambapo una faragha k kwa mfano ama nyumba yako ambapo unaweza Kiswahili; kujilaza na kupumzika kwa masaa machache baada ya kutumia dawa.
UKuwa na mtu mmoja ambaye ataweza kukupatia kama chai ya moto au kitu cha chakula na kukuangalia kama unapenda, inaweza ikasaidia.
Inashauriwa kunywa tembe za ibuprofen kabla ya kuitumia misoprostol kusaidia kupunguza maumivu
Hakikisha umeweka tayari mpango wa usalama kabla ya kutumia tembe za kuavya mimba, hili ni la muhimu iwapo utahitaji msaada wa matibabu ya dharura

Kutengeneza mpango wa usalama

Kulingana na shirika la Marekani la uzazi na jinakolojia, uavyaji wa mimba iliyo miezi mitatu au chini kwa kutumia tembe ni mojawapo ya taratibu za tiba salama . Hata hivyo, unapaswa kutayarisha ipasavyo kwa matibabu ya dharura kama itakavyohitajika. Zingatia maswali yetu hapa chini ili kusaidia kutengeneza mpango wako wa usalama iwapo kama utakavyohitaji.

Unahitaji kuwa na uwezo wa kufika kwenye kituo nkwa saa 1 au chini. (Kama una upungufu wa damu, unapaswa kuwa na uwezo wa kufika huko kwenye kituo kwa dakika 30.)

Je, kuna mtu atakayekuwa nawe na anayeweza kukufikisha kwa gari? Je, utachukua teksi? Utatumia Usafiri wa umma? Itagharimu pesa ngapi na je, inapatikana masaa ishirini na manne(24hours)? Kumbuka, sio salama kuendesha gari mwenyewe kwenda hospitalini wakati wa dharura ya matibabu.

Uavyaji wa mimba kutumia tembe una vikwazo vya kisheria nchini mwako? Ni nini utakachowaeleza wahudumu wa afya na madakatari ili waweze kuelewa msaada unaohitaji, huku ukilinda usalama na siri yako? Tuna baadhi ya mapendekezo iwapo unahitaji msaada wa taarifa na habari za kutoa inapohitajika.

Utakachowaambia wahudumu wa afya Katika baadhi ya nchi, kuavya mimba ukitumia tembe ni kinyume cha sheria. Hii ina maana kwambwa utakapohitaji msaada wa matibabu ya dharura, uwe mwangalifu unachosema. Kuavya mimba kw akutumia madawa kuna ishara sawa na mimba inayotoka kwa njia ya kawaida( pia hujulikana kama avyaji kwa hiari). Tumetayarisha baadhi ya majibu ambayo unaweza ukatumia:

  • Sina uhakika kinachoendelea , nimeanza kufuja damu kwa ghafla
  • Nina fuja damu lakini sidhani kwamba ni hedhi ya kawaida
  • Nimeanza kufuja damu kwa ghafla na ninahofu kwamba kuna shida

Marejeo:

HowToUseAbortionPill.org inashirikiana na shirika lisilo la faida lililosajiliwa huko Amerika-501c (3)
HowToUseAbortionPill.org hutoa yaliyomo yaliyokusudiwa kwa sababu ya habari tu na haihusiani na shirika la matibabu.